Wednesday, August 8, 2012

I wish this was true!


You have won a BMW X6 Concept 2011 model



Date: 08.08.2012
Subject: You have won BMW


Dear Sir,

You have won a BMW X6 Concept car 2011 model and and  £1,000,000.00 Pounds.

Contact Mr. Larry Quester with your:

Name...................
Country................
Age......................
Telephone.............


Mr. Larry Quester





Canoeist snags Norway's first Olympic gold

Eirik Verås Larsens. Photo: Junge/Heiko.

Eirik Verås Larsen paddled his way to the Norway's first gold medal of the 2012 London Olympics in the K1 1,0000 metre race on Wednesday.

The 36-year-old Norwegian claimed the fourth Olympic medal of his career after a dominant performance. When he rose up from the kayak, it was with a broad grin on his face.

"It's indescribable. Now I can retire with a clear conscience," he told NRK.

"I don't think it was going to happen. It has been a tough two years. To do this is fantastic."

Verås Larsen got a better start than expected and was at the front the whole way. Canadian Adam van Koeverden appeared the strongest for a while, but the Norwegian cam back strong in the final 250 metres.

The paddler from Flekkefjord crossed the line seven tenths of a second ahead of Van Koeverden, who ended up with silver. Bronze went to German Max Hoff.

The gold was Verås Larsen's second in the Olympic Games after winning the 1000-metre in Athens in 2004. In Beijing he claimed silver in the same distance and has taken a further bronze in the K2 1,000 metre event together with Nils Olav Fjeldheim in Athens

Team manager Jarle Aambø was rendered speechless by the veteran's second Olympic triumph.

"I am still a little shaky. My God what an incredible performer. I am speechless," Aambø said to NTB.
Source: NTB/The Local (news@thelocal.no)





Tuesday, August 7, 2012

Jumuia ya Watanzania; Norway, Sweden, Finland na Denmark



YAH:  HIFADHI YA JAMII KWA DIASPORA (WESTADI).

Kwa Jumuia ya Watanzania,

Ubalozi  wa Tanzania, Sweden, umepokea barua kutoka Wizara yetu ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ikitufahamisha kuhusu kuanzishwa kwa huduma ya HIFADHI YA JAMII KWA WATANZANIA WAISHIO NJE – Welfare Scheme for Tanzanians in the Diaspora (WESTADI).

Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) sasa imepanua huduma zake kwa Watanzania wanaoishi nje ya nchi kupitia Mpango wa Hifadhi ya Jamii kwa Watanzania waishio ughaibuni (Diaspora). Lengo la bima hii ni kuondoa adha kubwa inayoipata Diaspora kuhudumia ndugu wanapougua Tanzania, au diaspora anpougua akiwa likizo Tanzania na Mtanzania anapofariki akiwa nje ya nchi.

Chini ya WESTADI, mwanachana atatakiwa kulipa ada ya dola za Kimarekani mia tatu (USD 300) kwa mwaka ili kupata mafao kama ifuatavyo;

1.   Huduma va matibabu kwa wategemezi wanne (4) wa Mwanachana ambao wanaishi nyumbani (Tanzania);
2.   Huduma ya matibabu kwa Mwanachama pindi atakaposafiri kuja Tanzania wakati wa likizo au kwa sababu zozote zile;
3.   Huduma za kusafirisha mwili wa Mwanachama kuja nyumbani iwapo atafariki akiwa nje ya nchi pamoja na kulipia tiketi ya msindikizaji mmoja.
4.   Hudurna ya mazishi katika nchi anayoishi Mwanacharna ikiwa amechagua kuzikwa nchi aliyopo. 

Mtegemezi atachagua hospitali iliyo ndani ya mkoa husika na huduma kwake zitaanza mara moja baada ya kuthibitishwa kwa ingizo la pesa za Bima ya Mtu aliyeko nje.

Huduma zitasimama mara punde mwenye bima atakapositisha na kuondoa michango ya pesa za kila mwaka.

Ili kufahamu zaidi juu ya suala hili tafadhali rejea taarifa ya uzinduzi wa WESTADI uliofanyika Septemba 2011 wakati wa Kongamano lililoandaliwa na Watanzania waishio, Dikota, Marekani bofya (HAPA).  Mgeni wa heshima katika uzinduzi huu alikuwa Mh. Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Maelezo zaidi juu ya Mfuko huu na namna ya kuwa mwanachama yako katika tovuli ya NSSF (http://www.nssf.or.tz).

Pia kwa taarifa ya mfano kuonyesha faida ya mfuko huo kwa wanachama wake bofya hapa. (HAPA)

Ubalozi unaomba muisambaze taarifa hii kwa jumuia ya watanzania na muwasihi wawafahamishe na wengine. 

UBALOZI WA TANZANIA,
Näsby Allé 6
183 55 Täby

Simu: +46 8 732 24 30/31
Fax: +46 8 732 24 32
Baruapepe: mailbox@tanemb.se
SWEDEN

Ray Blaze (Nigeria), Jose Chameleone (Uganda) & Knowless (Rwanda)




Mais Marradas 5 Estrelas


Wahispania na mchezo wao wa kucheza na 
mang´ombe dume makali. Wana vichwa vya wendawazimu na roho za mawe!



Oslo, Norway



Monday, August 6, 2012


Mwanamziki wa Bongoflava, TID
kwenye Mkasi TV



Mchungaji Amani S. Golugwa (CHADEMA Arusha) alonga na Vijimambo





Mahojiano na Mheshimiwa Mbunge Zitto Kabwe aliyoyafanya na Fina Mango katika kipindi cha Makutano Agosti 4, 2012








TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUWEPO KWA MGONJWA WA EBOLA, WILAYA YA KARAGWE MKOA WA KAGERA, TANZANIA


Utangulizi

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapenda kutoa taarifa kwa umma, kuhusu tetesi zilizokuwa zimeenea hapa nchini kutoka kwenye vyombo mbali mbali vya habari kuhusu kuwepo kwa mgonjwa wa Ebola,wilayani Karagwe mkoa wa  Kagera.

Mnamo tarehe 3 Agosti 2012, Wizara ya Afya na Ustawi Wa Jamii ilipokea taarifa kutoka kwa mganga mkuu wa wilaya ya Karagwe ya kuwepo kwa mgonjwa aliyekuwa anahisiwa kuwa na dalili za ugonjwa wa Ebola, katika hospitali ya  Wilaya ya Nyakahanga. 

Aidha,taarifa hiyo ilibainisha kuwa mgonjwa huyo alikuwa ni mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka (6)  kutoka katika kijiji cha Nyakatundu wilayani Karagwe. Mgonjwa huyu alikuwa na dalili za homa kali, kulegea, kutokwa damu puani, kutapika damu,  na kukojoa damu.

Maelezo kutoka kwa mama mzazi zilieleza kuwa mtoto huyu alianza kuugua kuanzia tarehe 30 Agosti 2012, ambapo alipatiwa dawa ya Septrin baada ya hospitali binafsi kuonyesha kuwa ana  ugonjwa wa“Typhoid”.

Uchunguzi wa awali katika hospitali ya Nyakahanga ulionyesha kuwa mtoto huyu  alikuwa anasumbuliwa na uambukizo kwenye haja ndogo (Urinary Tract Infection).Vile vile alifanyiwa uchunguzi wa kimaabara na Vipimo vya malaria, Hepatitis na Typhoid havikuonyesha kuwepo  kwa magonjwa haya. Hospitali inaendelea kumpatia matibabu mtoto huyu na imewaweka mgonjwa na mama yake anayemtunza kwenye chumba maalum (Isolatiom room) kwa ajili ya uangalizi zaidi. 

Aidha mnamo tarehe 4 Agosti 2012, timu za wataalamu kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na timu ya mkoa wa Kagera imeweza kufika na kumfanyia uchunguzi wa kina pamoja na kuchukua sampuli za damu kwa ajili ya uchunguzi zaidi katika maabara ya Taifa ya uchunguzi wa magonjwa na Maabara za nje ya nchi, ili kubaini kama ameathirika na ugonjwa wa Ebola. 

Timu hiyo ya wataalamu imetoa taarifa kuwa hali ya mgonjwa huyu kwa sasa imeimarika ikiwa pamoja na kutokuwa na homa, kutapika na kukojoa damu kumekoma pia, uchunguzi uliofanywa kwa mama wa mtoto umeonyesha kuwa hana dalili zozote za ugonjwa wa Ebola.Vile vile hakuna taarifa ya mtu mwingine yeyote kwenye familia hiyo au kwenye maeneo ya kijiji hicho au cha jirani kuwa na dalili za ugonjwa huo.

Kufuatia taarifa hii, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na Mkoa wa Kagera imechukua hatua zifuatazo;

Imepeleka timu ya wataalamu mbali mbali kutoka Wizarani na mkoa  kwa lengo la kwenda kufuatilia na kutoa taarifa kuhusu kuwepo kwa ugonjwa huo. 
Imetoa elimu ya Afya kuhusu njia za kuzuia kuenea ugonjwa wa Ebola  pamoja na dalili za ugonjwa huu, kwa wananchi na watumishi wa afya katika hospitali ya Nyakahanga
Kupeleka vifaa kinga katika hospitali ya Nyakahanga pamoja na maeneo ya mipakani
Kutoa matangazo kwa jamii kwa kutumia vipaaza sauti na kupitia  radioni (Radio Karagwe) kuhusu ugonjwa huu.  Aidha, vipeperushi pia vimetolewa.

Hitimisho

Wizara inapenda kuufahamisha umma kuwa mpaka sasa hakuna mgonjwa yeyote aliyethibitishwa kuwa na ugonjwa wa Ebola hapa nchini.Aidha, Wizara ya Afya imejiaanda kikamilifu kukabiliana na ugonjwa huu iwapo utatokea hapa nchini.

Kwa sasa timu za wataalum  zipo katika mikoa ya Mara, Mwanza, Kagera, Kigoma, Kilimanjaro na Arusha, kutoa elimu juu ya ugonjwa huu kwa wataalamu na kwa wananchi na vilevile kufuatilia ugonjwa huu sehemu za mipakani.

Wizara inaendelea kutoa wito kwa wananchi kutoa taarifa haraka kwenye kituo chochote cha kutolea huduma za afya, mara wanapoona dalili za ugonjwa huu.


Imetolewa na:
kitengo cha Mawasiliano
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
Tarehe 6 Agosti, 2012.